18 Yesu alipokuwa anatembea kando ya ziwa Galilaya, aliwaona ndugu wawili wavuvi; Simoni (aitwae Petro) na Andrea, ndugu yake; walikuwa wakivua samaki kwa nyavu ziwani.19 Basi, akawaambia, "Nifuateni, nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. ic21 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona ndugu wengine wawili: Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Hao walikuwa ndani ya mashua pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Basi Yesu akawaita,22 nao mara wakaiacha mashua pamoja na baba yao, wakamfuata.
Publicidade
Mateus 4
Veja também
Publicidade