Aniversário
O aniversário é momento de celebrar a vida que Deus nos deu. A Bíblia nos convida a agradecer por cada dia, contar nossos anos com sabedoria e alegrar-se na bondade do Senhor.
Agradecer pela vida
Este é o dia que o Senhor fez — alegremo-nos! Cada dia é presente de Deus, cada ano é prova da sua fidelidade.
Hii ndiyo siku Mwenyezi Mungu aliyoifanya,
tushangilie na kufurahi ndani yake.
Msifuni Mwenyezi Mungu..
Mshukuruni Mwenyezi Mungu, kwa kuwa ni mwema;
fadhili zake zadumu milele.
Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu,
wala usisahau wema wake wote:
Ni vyema kumshukuru Mwenyezi Mungu
na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,
kuutangaza upendo wako asubuhi,
na uaminifu wako wakati wa usiku,
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi,
bali upendo wake hudumu siku zote.
Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha,
lakini furaha huja asubuhi.
Mpendwa, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kama vile roho yako ifanikiwavyo.
A obra de Deus em nós
Tu me teceste no ventre de minha mãe — maravilhosas são as tuas obras! Cada vida é obra-prima do Criador.
Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;
uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa
kwa namna ya ajabu na ya kutisha;
kazi zako ni za ajabu,
ninajua hayo kikamilifu.
Umbile langu halikufichika kwako,
nilipoumbwa mahali pa siri.
Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika.
Siku zangu zote ulizonipangia
ziliandikwa katika kitabu chako
kabla haijakuwa hata moja.
Tazama jinsi yalivyo ya thamani
mawazo yako kwangu, Ee Mungu!
Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!
Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;
uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa
kwa namna ya ajabu na ya kutisha;
kazi zako ni za ajabu,
ninajua hayo kikamilifu.
Umbile langu halikufichika kwako,
nilipoumbwa mahali pa siri.
Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika.
Siku zangu zote ulizonipangia
ziliandikwa katika kitabu chako
kabla haijakuwa hata moja.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe,
ulinitoa tumboni mwa mama yangu.
Nitakusifu wewe daima.
Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa,
toka tumboni mwa mama yangu
umekuwa Mungu wangu.
Hata hivyo ulinitoa tumboni,
ukanifanya nikutegemee,
hata nilipokuwa ninanyonya
matiti ya mama yangu.
Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa,
toka tumboni mwa mama yangu
umekuwa Mungu wangu.
Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Al-Masihi Isa.
Oração de bênção
O Senhor te abençoe e te guarde. Tu és toda formosa e em ti não há defeito. Deus cuida de cada detalhe da tua vida.
" ‘ "Mwenyezi Mungu akubariki
na kukulinda;
Mwenyezi Mungu akuangazie nuru ya uso wake
na kukufadhili;
Mwenyezi Mungu akugeuzie uso wake
na kukupa amani." ’
Wewe ni mzuri kote, mpendwa wangu,
hakuna hitilafu ndani yako.
Amevikwa nguvu na heshima,
anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.
Huzungumza kwa hekima,
na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.
Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu,
na uzuri unapita upesi;
bali mwanamke anayemcha Mwenyezi Mungu atasifiwa.
Mvi ni taji la utukufu;
hupatikana kwa maisha ya uadilifu.
Ninamshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo ninyi.
Sabedoria e alegria
Ensina-nos a contar os nossos dias. Deus encheu nosso cálice de alegria e o seu caminho mostra-se vida em plenitude.
Tufundishe kuzihesabu siku zetu vizuri,
ili tujipatie moyo wa hekima.
"Ee Mwenyezi Mungu, nijulishe mwisho wa maisha yangu
na hesabu ya siku zangu;
nijalie kujua jinsi maisha yangu
yanavyopita upesi.
Umefanya maisha yangu mafupi kama nyanda;
muda wangu wa kuishi ni kama
hauna thamani kwako.
Maisha ya kila mwanadamu
ni kama pumzi.
Umenijulisha njia ya uzima;
utanijaza na furaha mbele zako,
pamoja na furaha ya milele
katika mkono wako wa kuume.
Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa
kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
Jambo moja ninamwomba Mwenyezi Mungu,
hili ndilo ninalolitafuta:
niweze kukaa nyumbani mwa Mwenyezi Mungu
siku zote za maisha yangu,
niutazame uzuri wa Mwenyezi Mungu
na kumtafuta hekaluni mwake.
Hakika wema na upendo vitanifuata
siku zote za maisha yangu,
nami nitakaa nyumbani mwa Mwenyezi Mungu
milele.
Ahimidiwe Mwenyezi Mungu Mwamba wangu,
aifundishaye mikono yangu vita,
na vidole vyangu kupigana.
Yeye ni Mungu wangu wa upendo na ulinzi wangu,
ngome yangu na mwokozi wangu,
ngao yangu, ninayemkimbilia,
ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
Sasa nafahamu kuwa Mwenyezi Mungu
humwokoa mpakwa mafuta wake,
humjibu kutoka mbingu yake takatifu
kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.
Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi,
bali sisi tutalitumainia jina la Mwenyezi Mungu, Mungu wetu.
Wao wameshushwa chini na kuanguka,
bali sisi tunainuka na kusimama imara.
Mimi, Mwenyezi Mungu, ninalitunza,
ninalinywesha maji mfululizo.
Ninalichunga usiku na mchana
ili mtu yeyote asije akalidhuru.
Proteção e fidelidade
O Senhor pelejará por vós. Fiel é o Senhor que vos guarda — Ele te protege de todo mal o tempo todo.
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ndiye huenda pamoja nanyi kuwapigania dhidi ya adui zenu na kuwapatia ushindi."
Lakini Bwana Isa ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
Lakini Mungu apewe shukrani, yeye ambaye siku zote hutufanya tuandamane kwa ushindi tukiwa ndani ya Al-Masihi. Naye kupitia kwetu hueneza kila mahali harufu nzuri ya kumjua yeye.
Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Mwenyezi Mungu alilomwambia litatimizwa."