Publicidade

Aniversário

Por Bíblia Online

O aniversário é momento de celebrar a vida que Deus nos deu. A Bíblia nos convida a agradecer por cada dia, contar nossos anos com sabedoria e alegrar-se na bondade do Senhor.

Agradecer pela vida

Este é o dia que o Senhor fez — alegremo-nos! Cada dia é presente de Deus, cada ano é prova da sua fidelidade.

Hii ndiyo siku Mwenyezi Mungu aliyoifanya,

tushangilie na kufurahi ndani yake.

Wema wa Mwenyezi Mungu kwa watu wake

Msifuni Mwenyezi Mungu..

Mshukuruni Mwenyezi Mungu, kwa kuwa ni mwema;

fadhili zake zadumu milele.

Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu,

wala usisahau wema wake wote:

Wimbo wa kumsifu Mwenyezi Mungu

Ni vyema kumshukuru Mwenyezi Mungu

na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,

kuutangaza upendo wako asubuhi,

na uaminifu wako wakati wa usiku,

Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi,

bali upendo wake hudumu siku zote.

Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha,

lakini furaha huja asubuhi.

Gayo anatiwa moyo

Mpendwa, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema kama vile roho yako ifanikiwavyo.

A obra de Deus em nós

Tu me teceste no ventre de minha mãe — maravilhosas são as tuas obras! Cada vida é obra-prima do Criador.

Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;

uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.

Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa

kwa namna ya ajabu na ya kutisha;

kazi zako ni za ajabu,

ninajua hayo kikamilifu.

Umbile langu halikufichika kwako,

nilipoumbwa mahali pa siri.

Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,

macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika.

Siku zangu zote ulizonipangia

ziliandikwa katika kitabu chako

kabla haijakuwa hata moja.

Tazama jinsi yalivyo ya thamani

mawazo yako kwangu, Ee Mungu!

Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!

Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;

uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.

Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa

kwa namna ya ajabu na ya kutisha;

kazi zako ni za ajabu,

ninajua hayo kikamilifu.

Umbile langu halikufichika kwako,

nilipoumbwa mahali pa siri.

Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,

macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika.

Siku zangu zote ulizonipangia

ziliandikwa katika kitabu chako

kabla haijakuwa hata moja.

Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe,

ulinitoa tumboni mwa mama yangu.

Nitakusifu wewe daima.

Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa,

toka tumboni mwa mama yangu

umekuwa Mungu wangu.

Hata hivyo ulinitoa tumboni,

ukanifanya nikutegemee,

hata nilipokuwa ninanyonya

matiti ya mama yangu.

Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa,

toka tumboni mwa mama yangu

umekuwa Mungu wangu.

Shukrani

Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Al-Masihi Isa.

Oração de bênção

O Senhor te abençoe e te guarde. Tu és toda formosa e em ti não há defeito. Deus cuida de cada detalhe da tua vida.

" ‘ "Mwenyezi Mungu akubariki

na kukulinda;

Mwenyezi Mungu akuangazie nuru ya uso wake

na kukufadhili;

Mwenyezi Mungu akugeuzie uso wake

na kukupa amani." 

Wewe ni mzuri kote, mpendwa wangu,

hakuna hitilafu ndani yako.

Amevikwa nguvu na heshima,

anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.

Huzungumza kwa hekima,

na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.

Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu,

na uzuri unapita upesi;

bali mwanamke anayemcha Mwenyezi Mungu atasifiwa.

Mvi ni taji la utukufu;

hupatikana kwa maisha ya uadilifu.

Shukrani na maombi

Ninamshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo ninyi.

Sabedoria e alegria

Ensina-nos a contar os nossos dias. Deus encheu nosso cálice de alegria e o seu caminho mostra-se vida em plenitude.

Tufundishe kuzihesabu siku zetu vizuri,

ili tujipatie moyo wa hekima.

"Ee Mwenyezi Mungu, nijulishe mwisho wa maisha yangu

na hesabu ya siku zangu;

nijalie kujua jinsi maisha yangu

yanavyopita upesi.

Umefanya maisha yangu mafupi kama nyanda;

muda wangu wa kuishi ni kama

hauna thamani kwako.

Maisha ya kila mwanadamu

ni kama pumzi.

Umenijulisha njia ya uzima;

utanijaza na furaha mbele zako,

pamoja na furaha ya milele

katika mkono wako wa kuume.

Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa

kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.

Jambo moja ninamwomba Mwenyezi Mungu,

hili ndilo ninalolitafuta:

niweze kukaa nyumbani mwa Mwenyezi Mungu

siku zote za maisha yangu,

niutazame uzuri wa Mwenyezi Mungu

na kumtafuta hekaluni mwake.

Hakika wema na upendo vitanifuata

siku zote za maisha yangu,

nami nitakaa nyumbani mwa Mwenyezi Mungu

milele.

Mfalme amshukuru Mwenyezi Mungu kwa ushindi

Ahimidiwe Mwenyezi Mungu Mwamba wangu,

aifundishaye mikono yangu vita,

na vidole vyangu kupigana.

Yeye ni Mungu wangu wa upendo na ulinzi wangu,

ngome yangu na mwokozi wangu,

ngao yangu, ninayemkimbilia,

ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.

Sasa nafahamu kuwa Mwenyezi Mungu

humwokoa mpakwa mafuta wake,

humjibu kutoka mbingu yake takatifu

kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.

Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi,

bali sisi tutalitumainia jina la Mwenyezi Mungu, Mungu wetu.

Wao wameshushwa chini na kuanguka,

bali sisi tunainuka na kusimama imara.

Mimi, Mwenyezi Mungu, ninalitunza,

ninalinywesha maji mfululizo.

Ninalichunga usiku na mchana

ili mtu yeyote asije akalidhuru.

Proteção e fidelidade

O Senhor pelejará por vós. Fiel é o Senhor que vos guarda — Ele te protege de todo mal o tempo todo.

Kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ndiye huenda pamoja nanyi kuwapigania dhidi ya adui zenu na kuwapatia ushindi."

Lakini Bwana Isa ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.

Lakini Mungu apewe shukrani, yeye ambaye siku zote hutufanya tuandamane kwa ushindi tukiwa ndani ya Al-Masihi. Naye kupitia kwetu hueneza kila mahali harufu nzuri ya kumjua yeye.

Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.

Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Mwenyezi Mungu alilomwambia litatimizwa."

Seja o primeiro
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-