Confiar no Senhor
Confiar no Senhor é a base de toda vida espiritual. A confiança em Deus nos livra do medo, nos dá paz e nos posiciona para receber as promessas divinas.
Confiar de todo coração
Confia no Senhor de todo o coração. Não te apoies em teu próprio entendimento — em todos os caminhos o reconheça.
Mtumaini Mwenyezi Mungu kwa moyo wako wote
wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
katika njia zako zote mkiri yeye,
naye atayanyoosha mapito yako.
Mwenyezi Mungu mlinzi wetu
Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana,
atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Nitasema kumhusu Mwenyezi Mungu, "Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu, ninayemtumaini."
Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji,
na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
Atakufunika kwa manyoya yake,
chini ya mabawa yake utapata kimbilio,
uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
Usalama wa watu wa Mwenyezi Mungu
Wale wamtumainio Mwenyezi Mungu ni kama Mlima Sayuni,
ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,
ndivyo Mwenyezi Mungu anavyowazunguka watu wake
sasa na hata milele.
Hataogopa habari mbaya,
moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Mwenyezi Mungu.
Mtumaini Mwenyezi Mungu na utende yaliyo mema.
Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
Jifurahishe katika Mwenyezi Mungu
naye atakupa haja za moyo wako.
Mkabidhi Mwenyezi Mungu njia yako,
mtumaini yeye, naye atatenda hili:
Yeye atafanya haki yako ing’ae kama mapambazuko,
na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.
Wote wanaolijua jina lako watakutumaini wewe,
kwa maana wewe Mwenyezi Mungu,
hujawaacha kamwe wanaokutafuta.
Segurança em Deus
Bem-aventurado o homem que confia no Senhor. Ele é como árvore plantada junto às águas — não temerá quando vier o calor.
"Lakini amebarikiwa mtu anayemtumaini Mwenyezi Mungu,
ambaye matumaini yake ni katika Mwenyezi Mungu.
Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji
uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji.
Hauogopi wakati wa joto ujapo;
majani yake ni mabichi daima.
Hauna hofu katika mwaka wa ukame
na hautaacha kuzaa matunda."
Mtumaini Mwenyezi Mungu milele,
kwa kuwa Mwenyezi Mungu,
Mwenyezi Mungu,
ni Mwamba wa milele.
Hakika Mungu ni wokovu wangu;
nitamtumaini wala sitaogopa.
Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu,
ni nguvu zangu na wimbo wangu;
amekuwa wokovu wangu."
Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni,
heri mtu anayekutumaini wewe.
Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi,
bali sisi tutalitumainia jina la Mwenyezi Mungu, Mungu wetu.
Wao wameshushwa chini na kuanguka,
bali sisi tunainuka na kusimama imara.
Ni bora kumkimbilia Mwenyezi Mungu
kuliko kumtumainia mwanadamu.
Ni bora kumkimbilia Mwenyezi Mungu
kuliko kuwatumainia wakuu.
Não confiar no homem
Não temas — em ti confiarei. Melhor é confiar no Senhor do que confiar no homem ou nos príncipes.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu,
katika Mwenyezi Mungu, ambaye neno lake ninalisifu,
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa.
Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
Lakini ninategemea upendo wako usiokoma;
moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
Lakini mimi ninakutumaini wewe peke yako, Ee Mwenyezi Mungu;
nimesema, "Wewe ndiwe Mungu wangu."
Heri mtu yule amfanyaye Mwenyezi Mungu kuwa tumaini lake,
asiyewategemea wenye kiburi,
wale wenye kugeukia miungu ya uongo.
Isa awatia moyo wanafunzi wake
Isa akawaambia, "Msifadhaike mioyoni mwenu. Mnamwamini Mungu, mniamini pia.