Dia dos avós
Os avós são tesouros vivos de sabedoria e fé. A Bíblia honra os mais velhos e celebra a transmissão de fé entre gerações — dos avós aos netos e destes aos que virão.
A bênção dos avós
A coroa dos velhos são os filhos dos filhos. A misericórdia de Deus é de geração em geração sobre os que o temem.
Wana wa wana ndio taji la wazee,
Na utukufu wa watoto ni baba zao.
Bali fadhili za BWANA ni kwa wamchao
Tangu milele hata milele,
Na haki yake ni kwa vizazi vyote;
Nilikuwa kijana na sasa ni mzee,
Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa
Wala mzawa wake akiomba chakula.
Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako,
Kitayatangaza matendo yako makuu.
Maana BWANA ni mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake katika vizazi vyote.
Força e fidelidade
Mesmo na velhice darão frutos. Os cabelos brancos são coroa de glória. Deus não abandona seus filhos na idade avançada.
Watazaa matunda hadi wakati wa uzee,
Watajaa utomvu, watakuwa na ubichi.
Watangaze ya kuwa BWANA ni mwenye adili,
Mwamba wangu, ndani yake hamna udhalimu.
Kichwa chenye mvi ni taji la utukufu,
Kama kikionekana katika njia ya haki.
na hata uzee wenu mimi ndiye, na hata wakati wenu wa mvi nitawachukueni; nimefanya, nami nitachukua; naam, nitachukua na kuokoa.
Hata vijana watazimia na kuchoka, na vijana wanaume wataanguka; bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.
Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako;