Publicidade

Filhos

Por Bíblia Online

Os filhos são herança do Senhor — bênção e responsabilidade sagrada. A Bíblia orienta sobre a criação dos filhos com amor, disciplina e instrução nos caminhos de Deus.

Herança do Senhor

Os filhos são herança do Senhor e o fruto do ventre é seu galardão. Bem-aventurado o homem que enche deles a sua aljava.

Watoto ni urithi unaotoka kwa Mwenyezi Mungu,

uzao ni zawadi kutoka kwake.

Kama mishale mikononi mwa shujaa

ndivyo walivyo wana awazaao mtu katika ujana wake.

Heri mtu ambaye podo lake

limejazwa nao.

Hawataaibishwa wanaposhindana

na adui zao langoni.

Thawabu ya kumtii Mwenyezi Mungu

Heri wale wote wamchao Mwenyezi Mungu,

wanaoenda katika njia zake.

Utakula matunda ya kazi yako;

baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao

ndani ya nyumba yako;

wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni

kuizunguka meza yako.

Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchaye Mwenyezi Mungu.

Thawabu ya kumtii Mwenyezi Mungu

Heri wale wote wamchao Mwenyezi Mungu,

wanaoenda katika njia zake.

Utakula matunda ya kazi yako;

baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao

ndani ya nyumba yako;

wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni

kuizunguka meza yako.

Kisha wana wetu wakati wa ujana wao

watakuwa kama mimea iliyotunzwa vizuri,

binti zetu watakuwa kama nguzo zilizoviringwa

kurembesha jumba la kifalme.

Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi,

kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.

Mungu akawabariki na akawaambia, "Zaeni na mkaongezeke, mkaijaze dunia na kuitiisha. Mkatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kiendacho juu ya ardhi."

Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na mifugo wako wachanga, yaani ndama wa makundi yako ya ng’ombe, na wana-kondoo wa makundi yako.

Mtabarikiwa kuliko mataifa mengine yote, hakuna wanaume wala wanawake kwenu watakaokosa watoto, wala mifugo yenu haitakuwa tasa.

Instruir e disciplinar

Instrui a criança no caminho em que deve andar, e quando envelhecer não se desviará dele. Disciplina é amor em ação.

Mfundishe mtoto njia impasayo kuiendea,

naye hataiacha hata akiwa mzee.

Upumbavu umefungwa ndani ya moyo wa mtoto,

bali fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali naye.

Yeye asiyetumia fimbo yake hampendi mwanawe,

bali yeye ampendaye

huwa mwangalifu kumwadibisha.

Fimbo ya maonyo hutia hekima,

bali mtoto asiyeonywa humwaibisha mama yake.

Msemo 13

Usimnyime mtoto adhabu,

ukimwadhibu kwa fimbo, hatakufa.

Hekima ni bora kupita vyote

Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba;

sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.

Mithali za Sulemani:

Mwana mwenye hekima

huleta furaha kwa baba yake,

lakini mwana mpumbavu

huleta huzuni kwa mama yake.

Amri hizi ninazokupa leo zitakuwa katika moyo wako. Wafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo.

O amor de Deus por crianças

Deixai vir a mim as crianças. Jesus acolheu, abençoou e honrou as crianças como modelo de fé e humildade.

Isa alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, "Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.

Basi ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?

Naye Isa akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake,

ndivyo Mwenyezi Mungu anavyowahurumia wale wanaomcha;

Tazameni ni pendo kuu namna gani alilotupatia Baba, kwamba sisi tuitwe wana wa Mungu! Na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.

Bênção e promessa

O Senhor te abençoe e te guarde. Os filhos dos justos serão abençoados e suas gerações caminharão na retidão.

" ‘ "Mwenyezi Mungu akubariki

na kukulinda;

Mwenyezi Mungu akuangazie nuru ya uso wake

na kukufadhili;

Mwenyezi Mungu akugeuzie uso wake

na kukupa amani." 

Mungu na akupe umande wa mbinguni

na utajiri wa duniani:

wingi wa nafaka na divai mpya.

Mataifa yakutumikie,

na mataifa yakusujudie.

Uwe bwana juu ya ndugu zako,

na wana wa mama yako wakusujudie.

Walaaniwe wale wanaokulaani,

na wabarikiwe wale wanaokubariki."

Kwa maana nitamimina maji juu ya nchi yenye kiu,

na vijito vya maji juu ya ardhi iliyokauka;

nitamimina Roho wangu Mtakatifu juu ya watoto wako,

nayo baraka yangu juu ya wazao wako.

Nao watachipua kama nyasi katika shamba la majani,

kama mierezi kando ya vijito vya maji yanayotiririka.

Watoto wako wote watafundishwa na Mwenyezi Mungu,

nayo amani ya watoto wako itakuwa kuu.

"Kabla sijakuumba ndani ya tumbo la mama yako, nilikujua;

kabla hujazaliwa nilikutenga kwa kazi maalum;

nilikuweka uwe nabii kwa mataifa."

Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao. Nitawapa moyo mmoja na kutenda pamoja, ili waniche daima kwa mema yao wenyewe na kwa mema ya watoto wao baada yao.

Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;

uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.

Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa

kwa namna ya ajabu na ya kutisha;

kazi zako ni za ajabu,

ninajua hayo kikamilifu.

Umbile langu halikufichika kwako,

nilipoumbwa mahali pa siri.

Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,

macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika.

Siku zangu zote ulizonipangia

ziliandikwa katika kitabu chako

kabla haijakuwa hata moja.

Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa,

toka tumboni mwa mama yangu

umekuwa Mungu wangu.

Nilikuwa kijana na sasa ni mzee,

lakini sijaona kamwe wenye haki wameachwa

au watoto wao wakiombaomba chakula.

Wakati wote ni wakarimu na hukopesha bila masharti.

Watoto wao watabarikiwa.

Hatutayaficha kwa watoto wao;

tutakiambia kizazi kijacho

matendo yastahiliyo sifa ya Mwenyezi Mungu,

uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.

Wana wa wana ni taji la wazee,

nao wazazi ni fahari ya watoto wao.

Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama,

wamebarikiwa watoto wake baada yake.

Criação e obediência

Pais, criai vossos filhos na disciplina e instrução do Senhor. Filhos, obedecei a vossos pais — isto é justo e agradável a Deus.

Mafundisho kuhusu watoto na wazazi

Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana Isa, kwa kuwa hili ni jema. "Waheshimu baba yako na mama yako," hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi, "upate baraka na uishi siku nyingi duniani."

Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, bali waleeni kwa nidhamu na mafundisho ya Bwana Isa.

Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hii inampendeza Bwana Isa.

Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.

Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa Mwenyezi Mungu, Mungu wako.

Vumilieni taabu kwa ajili ya kufunzwa adabu. Mungu anawatendea ninyi kama watoto wake, kwa maana ni mtoto yupi asiyeadibishwa na mzazi wake? Kama hakuna kuadibishwa (ambalo ni fungu la watoto wote), basi ninyi ni watoto haramu, wala si watoto halali.

Kama mjane ana watoto ama wajukuu, hawa inawapasa awali ya yote wajifunze kutimiza wajibu wao wa kumcha Mungu katika matendo kwa kuwatunza wale wa jamaa zao wenyewe, na hivyo wawarudishie wema waliowatendea wazazi wao, kwa kuwa hivi ndivyo inavyompendeza Mungu.

Mwanamke anapokuwa na uchungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini baada ya mtoto kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha yake ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.

Watoto ambao mlisema wangechukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.

Seja o primeiro
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-