Louvor e adoração
O louvor e a adoração são o propósito supremo da vida cristã. A Bíblia está repleta de exortações a louvar o Senhor — com cânticos, instrumentos, danças e com todo o nosso ser.
Louvai ao Senhor!
Todo ser que respira louve ao Senhor! O louvor é o sacrifício agradável que oferecemos continuamente a Deus.
Kila chenye pumzi na kimsifu Mwenyezi Mungu.
Msifuni Mwenyezi Mungu!
Msifuni Mwenyezi Mungu..
Msifuni Mungu katika patakatifu pake,
msifuni katika mbingu zake kuu.
Msifuni kwa matendo yake makuu,
msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta,
msifuni kwa kinubi na zeze,
msifuni kwa matari na kucheza,
msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
msifuni kwa matoazi yaliayo,
msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
Kila chenye pumzi na kimsifu Mwenyezi Mungu.
Msifuni Mwenyezi Mungu!
msifuni kwa matari na kucheza,
msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
Na walisifu jina lake kwa kucheza
na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Msifuni Mwenyezi Mungu..
Mwimbieni Mwenyezi Mungu wimbo mpya,
sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Na walisifu jina lake kwa kucheza
na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Kwa maana Mwenyezi Mungu anapendezwa na watu wake,
anawavika wanyenyekevu taji la wokovu.
Watakatifu washangilie katika heshima hii,
na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Msifuni Mwenyezi Mungu..
Msifuni Mwenyezi Mungu kutoka mbinguni,
msifuni juu vileleni.
Msifuni, enyi malaika wake wote,
msifuni yeye, enyi jeshi lake lote la mbinguni.
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi,
msifuni yeye, enyi nyota zote zinazong’aa.
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu sana,
na ninyi maji juu ya anga.
Vilisifu jina la Mwenyezi Mungu
kwa maana aliamuru navyo vikaumbwa.
Aliviweka mahali pake milele na milele,
alitoa amri ambayo haibadiliki milele.
Msifuni Mwenyezi Mungu kutoka duniani,
ninyi wanyama wakubwa wa baharini,
na vilindi vyote vya bahari,
miali ya radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu,
pepo za dhoruba zinazotimiza amri zake,
ninyi milima na vilima vyote,
miti ya matunda na mierezi yote,
wanyama pori na mifugo yote,
viumbe vidogo na ndege warukao,
wafalme wa dunia na mataifa yote,
ninyi wakuu na watawala wote wa dunia,
vijana wa kiume na wanawali,
wazee na watoto.
Wote na walisifu jina la Mwenyezi Mungu,
kwa maana jina lake pekee limetukuka,
utukufu wake uko juu ya nchi na mbingu.
Basi kupitia kwa Isa, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Basi kupitia kwa Isa, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
Louvor como estilo de vida
Bendirei ao Senhor em todo tempo; o seu louvor estará sempre nos meus lábios. O louvor não depende de circunstâncias.
Nitamtukuza Mwenyezi Mungu nyakati zote,
sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu siku zote.
Nitamtukuza Mwenyezi Mungu nyakati zote,
sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu siku zote.
Nitamtukuza Mwenyezi Mungu nyakati zote,
sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu siku zote.
Nafsi yangu itajisifu katika Mwenyezi Mungu,
walioonewa watasikia na wafurahi.
Mtukuzeni Mwenyezi Mungu pamoja nami,
naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Lakini mimi nitatumaini siku zote;
nitakusifu zaidi na zaidi.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe,
ulinitoa tumboni mwa mama yangu.
Nitakusifu wewe daima.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako,
nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako,
nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha
ninapokuimbia sifa,
mimi, ambaye umenikomboa.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,
jina la Mwenyezi Mungu linapaswa kusifiwa.
shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndio mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Al-Masihi Isa.
Adoração em espírito e verdade
Os verdadeiros adoradores adorarão ao Pai em espírito e em verdade. Deus busca os que o adoram com coração sincero.
Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba anawatafuta watu wanaomwabudu kwa namna hii.
Mungu ni Roho, na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli."
Njooni, tumwimbie Mwenyezi Mungu kwa furaha;
tumfanyie kelele za shangwe
Mwamba wa wokovu wetu.
Tuje mbele zake kwa shukrani,
tumtukuze kwa vinanda na nyimbo.
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni Mungu mkuu,
mfalme mkuu juu ya miungu yote.
Mkononi mwake mna vilindi vya dunia,
na vilele vya milima ni mali yake.
Bahari ni yake, kwani ndiye aliyeifanya,
na mikono yake iliumba nchi kavu.
Njooni, tusujudu, tumwabudu,
tupige magoti mbele za Mwenyezi Mungu Muumba wetu,
Mpigieni Mwenyezi Mungu kelele za shangwe, dunia yote.
Mwabuduni Mwenyezi Mungu kwa furaha;
njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Mwabuduni Mwenyezi Mungu kwa furaha;
njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Ingieni malangoni mwake kwa shukrani
na katika nyua zake kwa kusifu,
mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
Mwimbieni Mwenyezi Mungu wimbo mpya;
mwimbieni Mwenyezi Mungu dunia yote.
Mwimbieni Mwenyezi Mungu, lisifuni jina lake;
tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Tangazeni utukufu wake katika mataifa,
matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;
yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,
lakini Mwenyezi Mungu aliziumba mbingu.
Fahari na enzi viko mbele yake;
nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Mpeni Mwenyezi Mungu, enyi jamaa za mataifa,
mpeni Mwenyezi Mungu utukufu na nguvu.
Mpeni Mwenyezi Mungu utukufu unaostahili jina lake;
leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Mwabuduni Mwenyezi Mungu katika uzuri wa utakatifu wake;
dunia yote na itetemeke mbele zake.
A grandeza de Deus
Grande é o Senhor e mui digno de louvor! Sua grandeza é insondável. Os céus declaram sua glória e toda a criação o adora.
Mwenyezi Mungu ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana,
ukuu wake haupimiki.
Hata hivyo umesimikwa kwenye kiti cha enzi,
Wewe Uliye Mtakatifu;
wewe ni sifa ya Israeli.
Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu,
katika kusanyiko nitakusifu wewe.
Ninyi ambao mnamcha Mwenyezi Mungu, msifuni!
Ninyi nyote wazao wa Yakobo, mheshimuni yeye!
Mcheni yeye, ninyi wazao wa Israeli!
Kwa maana hakupuuza wala kudharau
mateso ya aliyeteswa;
hakumficha uso wake
bali alisikiliza kilio chake.
Msifuni Mwenyezi Mungu..
Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa,
jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!
Msifuni Mwenyezi Mungu, kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni mwema,
liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Mwenyezi Mungu anatawala, nchi na ifurahi,
visiwa vyote vishangilie.
Furahini katika Mwenyezi Mungu, enyi wenye haki,
lisifuni jina lake takatifu.
"Mimi ndimi Mwenyezi Mungu; hilo ndilo Jina langu!
Sitampa mwingine utukufu wangu
wala sanamu sifa zangu.
Cânticos e instrumentos
Cantai ao Senhor um cântico novo! Louvai com salmos, hinos e cânticos espirituais, fazendo melodia no coração ao Senhor.
Neno la Al-Masihi na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
Neno la Al-Masihi na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana Isa mioyoni mwenu, siku zote mkimshukuru Mungu Baba Mwenyezi kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Isa Al-Masihi.
Mwimbieni Mwenyezi Mungu kwa furaha, enyi wenye haki;
wanyofu wa moyo wanapaswa kumsifu.
Msifuni Mwenyezi Mungu kwa kinubi,
mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Mwimbieni wimbo mpya;
pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Daudi pamoja na Waisraeli wote walikuwa wanasifu kwa nguvu zao zote mbele za Mungu, kwa nyimbo na kwa vinubi, zeze, matari, matoazi na tarumbeta.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa;
waambieni matendo yake yote ya ajabu.
Akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,
wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.
Wengi wataona na kuogopa
na kuweka tumaini lao kwa Mwenyezi Mungu.
Ni vyema kumshukuru Mwenyezi Mungu
na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,
Nitaimba kuhusu upendo wako na haki yako;
kwako wewe, Ee Mwenyezi Mungu, nitaimba sifa.
Nitaimba kuhusu upendo wako na haki yako;
kwako wewe, Ee Mwenyezi Mungu, nitaimba sifa.
Louvor nas lutas
Paulo e Silas louvaram na prisão e houve terremoto. O louvor é arma espiritual que transforma circunstâncias e derrota o inimigo.
Ilipokaribia usiku wa manane, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
Ilipokaribia usiku wa manane, Paulo na Sila walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Mwenyezi Mungu na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema:
"Mshukuruni Mwenyezi Mungu
kwa kuwa fadhili zake zadumu milele."
Walipoanza kuimba na kusifu, Mwenyezi Mungu akaweka waviziaji dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akasujudu na kuabudu, akasema:
"Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi,
nami nitaondoka uchi,
Mwenyezi Mungu alinipa,
naye Mwenyezi Mungu ameviondoa;
jina la Mwenyezi Mungu litukuzwe."
Mwimbieni Mwenyezi Mungu, enyi watakatifu wake;
lisifuni jina lake takatifu.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi,
bali upendo wake hudumu siku zote.
Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha,
lakini furaha huja asubuhi.
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza,
ulinivua gunia ukanivika shangwe,
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya.
Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wangu, nitakushukuru milele.
Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?
Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?
Weka tumaini lako kwa Mungu,
kwa kuwa bado nitamsifu,
Mwokozi wangu na Mungu wangu.
Nehemia akasema, "Nendeni mkafurahie chakula kizuri na vinywaji vitamu, na mpeleke sehemu kwa wale ambao hawana chochote cha kula. Siku hii ni takatifu kwa Mwenyezi Mungu. Msihuzunike, kwa kuwa furaha ya Mwenyezi Mungu ni nguvu zenu."
Gratidão e louvor
Em tudo dai graças. O louvor nasce da gratidão por quem Deus é e pelo que Ele faz. Cada bênção é motivo de adoração.
Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu.
Vyote vilivyo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.
Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu.
Vyote vilivyo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.
Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu,
wala usisahau wema wake wote:
Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu.
Vyote vilivyo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.
Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu,
wala usisahau wema wake wote:
akusamehe dhambi zako zote,
akuponya magonjwa yako yote,
aukomboa uhai wako na kaburi,
akuvika taji la upendo na huruma,
Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu,
wala usisahau wema wake wote:
Basi na wamshukuru Mwenyezi Mungu kwa upendo wake usiokoma,
na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu,
na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Mshukuruni Mwenyezi Mungu, liitieni jina lake;
wajulisheni mataifa aliyoyatenda.
Katika siku hiyo mtasema:
"Mshukuruni Mwenyezi Mungu, mliitie jina lake;
julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,
tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
Ee Mwenyezi Mungu, wewe ni Mungu wangu,
nitakutukuza na kulisifu jina lako,
kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu
umetenda mambo ya ajabu,
mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.
Ninakushukuru na kukuhimidi, Ee Mungu wa baba zangu:
Umenipa hekima na uwezo;
umenijulisha kile tulichokuomba,
umetujulisha ndoto ya mfalme."
A majestade do Rei
Ao nome de Jesus todo joelho se dobrará. A adoração culminará na eternidade, onde os redimidos louvarão ao Cordeiro para sempre.
Nao waliimba kwa sauti kuu, wakisema:
"Anastahili Mwana-Kondoo, yeye aliyechinjwa,
kupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu
na heshima na utukufu na sifa!"
Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, chini ya nchi, na baharini, na vyote vilivyomo, vikiimba:
"Sifa na heshima na utukufu na uweza
ni vyake yeye aliyeketi juu ya hicho kiti cha enzi,
na kwa Mwana-Kondoo,
milele na milele!"
Akasema kwa sauti kubwa, "Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji."
Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema:
"Msifuni Mungu wetu,
ninyi watumishi wake wote,
ninyi nyote mnaomcha,
wadogo kwa wakubwa!"
Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema:
"Msifuni Mungu wetu,
ninyi watumishi wake wote,
ninyi nyote mnaomcha,
wadogo kwa wakubwa!"
Kwa kuwa imeandikwa:
" ‘Kama vile niishivyo,’ asema Mwenyezi Mungu,
‘kila goti litapigwa mbele zangu,
na kila ulimi utakiri kwa Mungu.’ "
Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
Vida de louvor
O louvor transforma, fortalece a fé e nos conecta com o céu. Quem louva a Deus em toda circunstância experimenta sua presença real.
Mtumikieni Mwenyezi Mungu kwa hofu
na mshangilie kwa kutetemeka.
Nitamshukuru Mwenyezi Mungu kwa ajili ya haki yake,
na nitaliimbia sifa jina la Mwenyezi Mungu Aliye Juu Sana.
Ee Mwenyezi Mungu, nitakutukuza kwa moyo wangu wote,
nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
Ee Mwenyezi Mungu, nitakutukuza kwa moyo wangu wote,
nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
Nitafurahi na kushangilia ndani yako.
Nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana.
Ahimidiwe Mwenyezi Mungu,
kwa maana amesikia kilio changu
nikimwomba anihurumie.
Mwenyezi Mungu ni nguvu zangu na ngao yangu,
moyo wangu umemtumaini yeye,
nami nimesaidiwa.
Moyo wangu unarukaruka kwa furaha
nami nitamshukuru kwa wimbo.
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi,
naye aiandaa njia yake
ili nimwoneshe wokovu wa Mungu."
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu,
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa.
Mwanadamu mwenye kufa
atanitenda nini?
Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa.
Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
Mungu unayenipenda.
Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai,
midomo yangu itakuadhimisha.
Nitakusifu siku zote za maisha yangu,
na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;
kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
Ewe usikiaye maombi,
watu wote watakuja kwako wewe.
Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,
wewe ulisamehe makosa yetu.
Nilimlilia kwa kinywa changu,
sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.
Ahimidiwe Mungu,
ambaye hakulikataa ombi langu,
wala kunizuilia upendo wake!
Bali wenye haki na wafurahi,
washangilie mbele za Mungu,
wafurahi na kushangilia.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake,
mtukuzeni yeye anayepita juu ya mawingu:
jina lake ni Mwenyezi Mungu,
furahini mbele zake.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane,
ni Mungu katika makao yake matakatifu.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake,
mtukuzeni yeye anayepita juu ya mawingu:
jina lake ni Mwenyezi Mungu,
furahini mbele zake.
Ahimidiwe Bwana, Mungu Mwokozi wetu,
ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe,
wanaotembea katika mwanga
wa uwepo wako, Ee Mwenyezi Mungu.
Sio kwetu sisi, Ee Mwenyezi Mungu, sio kwetu sisi,
bali utukufu ni kwa jina lako,
kwa sababu ya upendo
na uaminifu wako.
Msifuni Mwenyezi Mungu, enyi mataifa yote;
mtukuzeni yeye, enyi watu wote.
Kwa kuwa upendo wake kwetu ni mkuu,
uaminifu wa Mwenyezi Mungu unadumu milele.
Msifuni Mwenyezi Mungu.
Nitakusifu kwa moyo mnyofu
ninapojifunza sheria zako za haki.
Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani;
uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa
kwa namna ya ajabu na ya kutisha;
kazi zako ni za ajabu,
ninajua hayo kikamilifu.
Ahimidiwe Mwenyezi Mungu Mwamba wangu,
aifundishaye mikono yangu vita,
na vidole vyangu kupigana.
Msifuni Mwenyezi Mungu!.
Ee nafsi yangu, umsifu Mwenyezi Mungu,
Nitamsifu Mwenyezi Mungu maisha yangu yote;
nitamwimbia Mungu wangu sifa
wakati wote ningali hai.
Lakini Mungu apewe shukrani, yeye ambaye siku zote hutufanya tuandamane kwa ushindi tukiwa ndani ya Al-Masihi. Naye kupitia kwetu hueneza kila mahali harufu nzuri ya kumjua yeye.
alitangulia kutuchagua tuwe wanawe kupitia kwa Isa Al-Masihi kwa furaha na mapenzi yake. Kwa hiyo tunamsifu Mungu kwa huruma zake kuu alizotumiminia sisi katika Mwanawe Mpendwa.
Namwomba Mungu awaimarishe kwa kuwatia nguvu mioyo yenu kupitia kwa Roho wake Mtakatifu kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake,
Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu walio milki ya Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa zake yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.
Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu walio milki ya Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa zake yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu. Mwanzo ninyi mlikuwa si taifa, lakini sasa ninyi ni taifa la Mungu. Mwanzo mlikuwa hamjapata rehema, lakini sasa mmepata rehema.
"Ninamwita Mwenyezi Mungu, anayestahili kusifiwa,
nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Mwenyezi Mungu, kati ya mataifa;
nitaliimbia sifa jina lako.
Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.
Atasema: "Sikia, ee Israeli, leo unaenda vitani kupigana na adui zako. Usife moyo wala usiogope, usitishwe wala usitiwe hofu mbele yao.
Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haistahili kuwa hivyo.
Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitajenga jumuiya ya wafuasi wangu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kuwashinda.
Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Al-Masihi Isa.
Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
Pigana vile vita vizuri vya imani. Shika uzima wa milele ambao ndio ulioitiwa ulipokiri ule ukiri mzuri mbele ya mashahidi wengi.
Nawaandikia ninyi akina baba,
kwa sababu mmemjua
yeye aliye tangu mwanzo.
Nawaandikia ninyi vijana,
kwa sababu mna nguvu,
na neno la Mungu linakaa ndani yenu,
nanyi mmemshinda yule mwovu.
Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe, wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kundi la waumini wa Isa wale waliokuwa wakiokolewa.