Paciência
A paciência é fruto do Espírito e virtude essencial da vida cristã. Deus é paciente conosco, e nos chama a ser pacientes com os outros e nas provações.
A paciência de Deus
Deus é clemente e tardio em irar-se. Sua paciência revela seu desejo de que todos se arrependam e cheguem ao conhecimento da verdade.
BWANA amejaa huruma na neema,
Haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili.
Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyodhani anakawia, bali huwavumilia, maana hapendi mtu yeyote apotee, bali wote wafikie toba.
Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.
rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi kuadhibu.
Lakini kwa ajili hii nilipata rehema, ili katika mimi wa kwanza, Yesu Kristo audhihirishe uvumilivu wake wote; niwe kielelezo kwa wale watakaomwamini baadaye, wapate uzima wa milele.
Ahadi ya Mungu kwa Sayuni
Kwa ajili ya hayo BWANA atangoja, ili awaonee huruma, na kwa ajili ya hayo atatukuzwa, ili awarehemu; kwa maana BWANA ni Mungu wa hukumu; heri wote wamngojao.
Esperar com paciência
Os que esperam no Senhor renovam as forças. A paciência produz caráter, e o caráter produz esperança que não decepciona.
Umtumainie BWANA, uwe imara,
Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.
Utulie mbele za BWANA,
Nawe umngojee kwa subira;
Usihangaike juu ya afanikiwaye katika njia yake,
Wala mtu apangaye maovu.
BWANA, asubuhi utaisikia sauti yangu,
Asubuhi nitakupangia dua yangu na kutazamia.
Bali tukikitumainia kitu tusichokiona, twakingojea kwa subira.
kwa tumaini, mkifurahi; katika dhiki, mkisubiri; mkidumu katika kusali;
BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.
Paciência nas provações
O amor é paciente. A paciência é marca de maturidade espiritual e nos permite perseverar mesmo quando as circunstâncias são adversas.
Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.
Na Mungu mwenye saburi na faraja awajalie kunuia mamoja ninyi kwa ninyi, kwa kufuata mfano wa Kristo Yesu;
kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo;
Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,
lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.
Perseverança até o fim
Quem perseverar até o fim será salvo. O domínio próprio é maior que a conquista de uma cidade.
Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.
Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu.
Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa;
Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.
Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi;
Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.
Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako.
Maana ghadhabu zake ni za muda mfupi tu;
Radhi yake ni ya milele.
Kilio huweza kuwapo usiku,
Lakini furaha huja asubuhi.