Seguir a Jesus
Seguir a Jesus é o convite mais transformador da Bíblia. Jesus chamou pescadores, cobradores de impostos e pessoas comuns para deixar tudo e segui-lo. Esse chamado continua vivo hoje.
O chamado de Jesus
Jesus disse: 'Segue-me'. Esse convite simples e poderoso mudou a vida de pescadores, publicanos e pessoas comuns ao longo da história.
Isa akawaambia, "Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu." Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
Isa amwita Mathayo
Isa alipokuwa akienda kutoka huko, alimwona mtu mmoja jina lake Mathayo akiwa ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru. Isa akamwambia, "Nifuate." Mathayo akasimama, akamfuata.
Siku iliyofuata Isa aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, "Nifuate."
Gharama ya kumfuata Isa
Walipokuwa njiani wakienda, mtu mmoja akamwambia Isa, "Nitakufuata popote utakakoenda."
Isa akamjibu, "Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake."
Isa akamwambia mtu mwingine, "Nifuate."
Mtu huyo akamjibu, "Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu."
Isa akamwambia, "Waache wafu wawazike wafu wao, bali wewe nenda ukautangaze ufalme wa Mungu."
Mtu mwingine akamwambia, "Bwana, nitakufuata lakini naomba kwanza nikawaage jamaa zangu."
Isa akamwambia, "Mtu yeyote ashikaye jembe kulima kisha akatazama nyuma hafai kwa ufalme wa Mungu."
O custo do discipulado
Seguir a Jesus exige renúncia. É preciso tomar a cruz diariamente, deixar tudo para trás e amar a Cristo acima de qualquer outro vínculo.
Ndipo Isa akawaambia wanafunzi wake, "Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
"Mtu yeyote anayekuja kwangu hawezi kuwa mwanafunzi wangu kama hatanipenda mimi zaidi ya baba yake na mama yake, mke wake na watoto wake, ndugu zake na dada zake, naam, hata maisha yake mwenyewe. Yeyote asiyeuchukua msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.
Ndipo Petro akamjibu, "Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!"
Isa akasema, "Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza."
Caminhar com Cristo
Quem segue a Jesus não anda em trevas, mas tem a luz da vida. Ele nos convida a crescer nele e a servir como Ele serviu.
Isa nuru ya ulimwengu
Kisha Isa akasema nao tena, akawaambia, "Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata, hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima."
Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
Mfano wa mateso ya Al-Masihi
Ninyi mliitwa kwa ajili ya haya, kwa sababu Al-Masihi naye aliteswa kwa ajili yenu, akiwaachia kielelezo, ili mzifuate nyayo zake.
"Yeye hakutenda dhambi,
wala hila haikuonekana kinywani mwake."
Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutishia, bali alijikabidhi kwa yeye ahukumuye kwa haki.
Badala yake, tukiambiana kweli kwa upendo, katika mambo yote tukue, hata tumfikie yeye aliye kichwa, yaani Al-Masihi.
Ni lazima mzitii sheria zangu, na mwe waangalifu kuzifuata amri zangu. Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.