4 akamwambia, "Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama juu ya vipaji vya nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu."
5 Nikiwa ninasikia, akawaambia wale wengine, "Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko. 6 Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wanawake na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu." Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.