Pular para o conteúdo
Publicidade

Yoshua 12

Orodha Ya Wafalme Walioshindwa

1 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:

2 Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.

Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi. 3 Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi12:3 Yaani Bahari ya Galilaya. hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi12:3 Yaani Bahari Mfu.), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.

4 Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.

5 Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.

6 Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.

7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao: 8 nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):

9 mfalme wa Yeriko mmoja

mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja

10 mfalme wa Yerusalemu mmoja

mfalme wa Hebroni mmoja

11 mfalme wa Yarmuthi mmoja

mfalme wa Lakishi mmoja

12 mfalme wa Egloni mmoja

mfalme wa Gezeri mmoja

13 mfalme wa Debiri mmoja

mfalme wa Gederi mmoja

14 mfalme wa Horma mmoja

mfalme wa Aradi mmoja

15 mfalme wa Libna mmoja

mfalme wa Adulamu mmoja

16 mfalme wa Makeda mmoja

mfalme wa Betheli mmoja

17 mfalme wa Tapua mmoja

mfalme wa Heferi mmoja

18 mfalme wa Afeki mmoja

mfalme wa Lasharoni mmoja

19 mfalme wa Madoni mmoja

mfalme wa Hazori mmoja

20 mfalme wa Shimron-Meroni mmoja

mfalme wa Akishafu mmoja

21 mfalme wa Taanaki mmoja

mfalme wa Megido mmoja

22 mfalme wa Kedeshi mmoja

mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja

23 mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) 12:23 Au: katika miinuko ya Nafoth-Dori. mmoja

mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja

24 mfalme wa Tirsa mmoja

wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também