Publicidade

1 Pedro 2

4 Mnapokuja kwake, yeye aliye Jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu bali kwa Mungu ni teule na la thamani kwake, 5 ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mnajengwa kuwa nyumba ya kiroho, ili mpate kuwa ukuhani mtakatifu, mkitoa dhabihu za kiroho zinazokubaliwa na Mungu kupitia kwa Isa Al-Masihi. 6 Kwa maana imeandikwa katika Maandiko:

"Tazama, naweka katika Sayuni,

jiwe la pembeni teule lenye thamani,

na yeyote atakayemwamini

hataaibishwa kamwe."

7 Kwenu ninyi mnaoamini, jiwe hili ni la thamani. Lakini kwao wasioamini,

"Jiwe walilolikataa waashi

limekuwa jiwe kuu la pembeni,"

8 tena,

"Jiwe lenye kuwafanya watu wajikwae,

na mwamba wa kuwaangusha."

Wanajikwaa kwa sababu hawakulitii lile neno, kama walivyowekewa tangu zamani.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-29_22-07-56-