20 Kisha Al-Yasa akawaacha maksai wake, akamkimbilia Ilya, akamwambia, "Niruhusu nikawabusu baba yangu na mama yangu, halafu nitafuatana nawe."
Ilya akajibu, "Rudi zako, kwani nimekufanya nini?"
21 Basi Al-Yasa akamwacha Ilya, naye akarudi. Akachukua ile jozi yake ya maksai na kuwachinja. Akaipika ile nyama kwa kutumia miti ya nira kama kuni na kuwapa watu, nao wakala. Kisha akaondoka, akamfuata Ilya, akamtumikia.