20 Kwa maana ahadi zote za Mungu zilizo katika Al-Masihi ni "Ndiyo". Kwa sababu hii, ni kwake yeye tunasema "Amen" kwa utukufu wa Mungu. 21 Basi ni Mungu atufanyaye sisi pamoja nanyi kusimama imara katika Al-Masihi. Alitupaka mafuta 22 kwa kututia muhuri wake na kutupatia Roho wake Mtakatifu mioyoni mwetu kuwa rehani kwa ajili ya kututhibitishia yote aliyotuahidi.