21 Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Mwenyezi Mungu na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema:
"Mshukuruni Mwenyezi Mungu
kwa kuwa fadhili zake zadumu milele."
22 Walipoanza kuimba na kusifu, Mwenyezi Mungu akaweka waviziaji dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.