5 Mawimbi ya mauti yalinizunguka,
mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 Kamba za Kuzimu22:6 Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, yaani Shimo lisilo na mwisho. zilinizunguka,
mitego ya mauti ilinikabili.
7 "Katika shida yangu nalimwita Mwenyezi Mungu,
nilimlilia Mungu wangu.
Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu,
kilio changu kikafika masikioni mwake.