Pular para o conteúdo
Publicidade

2 Samweli 5

Daudi atawazwa mfalme wa Israeli

1 Makabila yote ya Israeli yakamjia Daudi huko Hebroni na kumwambia, "Sisi tu mwili wako na damu yako. 2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme juu yetu, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani. Naye Mwenyezi Mungu alikuambia, Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’ "

3 Wazee wote wa Israeli wakamwendea Mfalme Daudi huko Hebroni, mfalme akafanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Mwenyezi Mungu, nao wakampaka Daudi mafuta kuwa mfalme wa Israeli.

Veja também