Kwa kundi la waumini lililoko Sardi
1 "Kwa malaika wa kundi la waumini lililoko Sardi, andika:
Haya ndio maneno ya aliye na zile Roho saba za Mungu3:1 Roho saba za Mwenyezi Mungu hapa inamaanisha Roho wa Mungu katika ukamilifu wa utendaji wake. na zile nyota saba.
Nayajua matendo yako, kwamba una sifa ya kuwa hai, lakini umekufa. 2 Amka! Nawe uyaimarishe yale yaliyosalia na yaliyo karibu kufa, kwa maana sikuona kwamba kazi zako zimekamilika machoni pa Mungu wangu.