16 Kamwe hawataona njaa
wala kiu tena.
Jua halitawachoma
wala joto lolote liunguzalo.
17 Kwa maana Mwana-Kondoo
aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi
atakuwa Mchungaji wao;
naye atawaongoza kwenda
kwenye chemchemi za maji yaliyo hai.
Naye Mungu atawafuta machozi
kutoka machoni mwao."