Paulo na Sila watiwa gerezani
16 Siku moja, tulipokuwa tukienda mahali pa kusali, tulikutana na mjakazi aliyekuwa na pepo wa uaguzi. Naye alikuwa amewapa mabwana zake mapato makubwa ya fedha kwa ubashiri. 17 Huyu mjakazi alikuwa akimfuata Paulo na sisi akipaza sauti na kusema, "Watu hawa ni watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, wao wanawatangazieni njia ya wokovu." 18 Akaendelea kufanya hivi kwa siku nyingi, lakini Paulo akiwa ameudhika sana, akageuka na kumwambia yule pepo mchafu, "Ninakuamuru katika jina la Isa Al-Masihi, umtoke!" Yule pepo mchafu akamtoka mara hiyo.