Petro ahutubia umati
14 Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akapaza sauti yake na kuhutubia umati ule wa watu, akasema: "Wayahudi wenzangu na nyote mnaoishi Yerusalemu, nisikilizeni kwa makini, ili jambo hili lijulikane kwenu. 15 Hakika watu hawa hawajalewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi! 16 La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:
17 " ‘Katika siku za mwisho, asema Mungu,
nitamimina Roho wangu
juu ya wote wenye mwili.
Wana wenu wa kiume na wa kike watatabiri,
vijana wenu wataona maono,
na wazee wenu wataota ndoto.