36 Walipokuwa wakiendelea na safari wakafika mahali palipokuwa na maji, yule towashi akamuuliza Filipo, "Tazama, hapa kuna maji. Kitu gani kitanizuia nisibatizwe?"
[ 37 8:37 Maandiko mengine ya kale hayana aya hii.Filipo akamwambia, "Ukiamini kwa moyo wako wote, unaweza kubatizwa."
Akajibu, "Naamini kuwa Isa Al-Masihi ni Mwana wa Mungu."] 38 Naye akaamuru lile gari lisimamishwe. Filipo na yule towashi wakateremka kwenye maji pamoja, naye Filipo akambatiza.