Pular para o conteúdo
Publicidade

Colossenses 1

12 mkimshukuru Baba, ambaye amewastahilisha kushiriki katika urithi wa watakatifu katika ufalme wa nuru. 13 Kwa maana ametuokoa kutoka ufalme wa giza na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake Mpendwa, 14 ambaye kwake tunao ukombozi, yaani msamaha wa dhambi.

Ukuu wa Al-Masihi

15 Yeye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. 16 Kwake yeye vitu vyote vilivyo mbinguni na juu ya nchi viliumbwa: vitu vinavyoonekana na visivyoonekana, viwe ni viti vya utawala au falme, au wenye mamlaka au watawala; vitu vyote viliumbwa kupitia kwake na kwa ajili yake. 17 Yeye alikuwako kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja.

Veja também

Colossenses
Ver todos os capítulos de Colossenses