6 Abramu akamwambia, "Haya, mtumishi wako yuko mkononi mwako. Mtendee lolote utakalo!" Ndipo Sarai akamtesa Hajiri, naye akamtoroka.
7 Malaika wa Mwenyezi Mungu akamkuta Hajiri karibu na chemchemi huko jangwani; chemchemi hiyo ilikuwa kando ya barabara iendayo Shuri. 8 Malaika akamwambia, "Hajiri, mtumishi wa Sarai, umetoka wapi, na unaenda wapi?"
Akamjibu, "Ninamkimbia bibi yangu Sarai."