10 Kisha Mwenyezi Mungu akasema, "Hakika nitakurudia majira kama haya mwaka ujao, na Sara mkeo atakuwa na mwana."
Sara alikuwa akiwasikiliza kwenye ingilio la hema lililokuwa nyuma ya Ibrahimu. 11 Ibrahimu na Sara walikuwa wazee tena waliosogea miaka, naye Sara alikuwa amepita umri wa kuzaa mtoto. 12 Hivyo Sara akacheka kimoyomoyo alipokuwa akiwaza, "Baada ya mimi kuwa mkongwe hivi na bwana wangu amezeeka, je, nitaweza kufurahia jambo hili?"