17 Akamwambia Adamu, "Kwa sababu umemsikiliza mke wako na ukala kutoka mti niliokuamuru, ‘Msile tunda lake,’
"Ardhi imelaaniwa kwa sababu yako;
kwa kazi ngumu utakula chakula kitokacho humo
siku zote za maisha yako.
18 Itakuzalia miiba na mibaruti,
nawe utakula mimea ya shambani.
19 Kwa jasho la uso wako
utakula chakula chako
hadi utakaporudi ardhini,
kwa kuwa ulitwaliwa kutoka humo;
wewe u mavumbi
na mavumbini utarudi."