7 Nuhu na mkewe, na wanawe na wake zao, wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika. 8 Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vinavyotambaa ardhini, 9 wa kiume na wa kike, walikuja kwa Nuhu, wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Nuhu. 10 Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
Publicidade