4 "Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu, kwa maana damu ni uhai. 5 Hakika damu ya uhai wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila mnyama. Kutoka kwa kila mwanadamu pia nitaidai kwa ajili ya uhai wa binadamu mwenzake.
6 "Yeyote amwagaye damu ya mwanadamu,
damu yake itamwagwa na mwanadamu;
kwa kuwa katika mfano wa Mungu,
Mungu alimuumba mwanadamu.