Dhabihu ya Al-Masihi ni mara moja tu
1 Torati ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kupitia kwa dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu. 2 Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi. 3 Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka, 4 kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.