Isa awatia moyo wanafunzi wake
1 Isa akawaambia, "Msifadhaike mioyoni mwenu. Mnamwamini Mungu, mniamini pia. 2 Nyumbani mwa Baba yangu kuna makao mengi. Kama sivyo, ningewaambia. Naenda kuwaandalia makao. 3 Nami nikienda na kuwaandalia makao, nitarudi tena na kuwachukua mkae pamoja nami, ili mahali nilipo nanyi mpate kuwepo.