4 Pilato akatoka tena nje, akawaambia wale waliokusanyika, "Tazameni, namkabidhi Isa kwenu kuwajulisha kwamba mimi sioni msingi wowote wa kumshtaki." 5 Kwa hiyo Isa akatoka nje akiwa amevaa lile taji la miiba na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, "Tazameni, mtu ndiye huyu!"
6 Wale viongozi wa makuhani na maafisa walipomwona, wakapiga kelele wakisema, "Msulubishe! Msulubishe!"
Pilato akawaambia, "Mchukueni ninyi mkamsulubishe. Lakini mimi sioni msingi wowote wa kumshtaki."