16 Isa akamwita, "Mariamu!"
Ndipo Mariamu akamgeukia Isa na kusema naye kwa Kiebrania, "Raboni!" (maana yake "Mwalimu").
17 Isa akamwambia, "Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba20:17 Yaani Mwana wa asili moja na Mwenyezi Mungu (Yohana 1:1-2), wa kiroho, bali si wa kimwili.. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ‘Ninapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu ambaye ni Mungu wenu.’ "
18 Kwa hiyo Mariamu Magdalene akaenda kuwatangazia wanafunzi wa Isa, akisema, "Nimemwona Bwana!" Naye akawaambia kwamba Isa alikuwa amemweleza mambo hayo yote.