19 Wanafunzi walipokuwa wameenda mwendo wa maili tatu au nne6:19 kama kilomita 5 au 6, walimwona Isa akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana. 20 Lakini Isa akawaambia, "Ni mimi. Msiogope." 21 Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.