28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: "Salamu, wewe uliyebarikiwa, Mwenyezi Mungu yu pamoja nawe!"
29 Mariamu akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni salamu hii ni ya namna gani. 30 Ndipo malaika akamwambia, "Usiogope, Mariamu; umepata kibali kwa Mungu. 31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto wa kiume na utamwita jina Isa.