Pular para o conteúdo
Publicidade

Lucas 1

Wimbo wa Mariamu

46 Naye Mariamu akasema:

"Moyo wangu wamwadhimisha Mwenyezi Mungu,

47 nayo roho yangu inamfurahia

Mungu Mwokozi wangu,

48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili

unyonge wa mtumishi wake.

Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,

49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu

amenitendea mambo ya ajabu:

jina lake ni takatifu.

50 Rehema zake hudumu kizazi hadi kizazi,

kwa wale wanaomcha.

51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake;

amewatawanya wale wenye kiburi

ndani ya mioyo yao.

52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya utawala,

lakini amewainua wanyenyekevu.

53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri,

bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.

54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli,

kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu

55 Ibrahimu na uzao wake milele,

kama alivyowaahidi baba zetu."

Veja também