Pular para o conteúdo
Publicidade

Lucas 1

Unabii wa Zakaria

67 Zakaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu wa Mungu, naye akatoa unabii, akisema:

68 "Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli,

kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.

69 Naye ametusimamishia pembe1:69 pembe inamaanisha nguvu ya wokovu

katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,

70 (kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake

watakatifu tangu zamani),

71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu,

na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:

72 ili kuonesha rehema kwa baba zetu

na kukumbuka agano lake takatifu,

73 kiapo alichomwapia baba yetu Ibrahimu:

74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu,

tupate kumtumikia yeye pasipo hofu

75 katika utakatifu na haki mbele zake,

siku zetu zote.

76 "Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana;

kwa kuwa utamtangulia Mwenyezi Mungu

na kuandaa njia kwa ajili yake,

77 kuwajulisha watu wake wokovu

utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,

78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu,

nuru inayotoka juu itatuzukia

79 ili kuwaangazia wale wanaoishi gizani

na katika uvuli wa mauti,

kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani."

Veja também