11 Wakati huo huo akaja mwanamke mmoja aliyekuwa na pepo mchafu, naye alikuwa amepinda mgongo kwa muda wa miaka kumi na nane, wala alikuwa hawezi kunyooka wima. 12 Isa alipomwona, akamwita, akamwambia, "Mwanamke, uwe huru, umepona ugonjwa wako." 13 Isa alipomwekea mikono yake, akasimama wima mara moja, akaanza kumtukuza Mungu.