Kuja kwa Ufalme wa Mwenyezi Mungu
20 Isa alipoulizwa na Mafarisayo17:20 Kundi la kidini la Wayahudi; walifuata Torati kwa dhati, hasa maagizo kuhusu utakaso. Pia waliamini katika malaika, ufufuo wa wafu, na kuja kwa Masihi ambaye atarejesha ufalme wa Daudi na ukuu wa taifa la Israeli. ufalme wa Mungu utakuja lini, yeye akawajibu, "Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza kwa bidii, 21 wala watu hawatasema, ‘Huu hapa,’ au ‘Ule kule,’ kwa maana ufalme wa Mungu umo ndani yenu."