Pular para o conteúdo
Publicidade

Lucas 19

Zakayo mtoza ushuru

1 Isa akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji. 2 Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo. 3 Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Isa ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza, kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo. 4 Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Isa, kwa sababu angeipitia njia ile.

5 Isa alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, "Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani mwako!" 6 Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Isa nyumbani mwake kwa furaha kubwa.

7 Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunung’unika wakisema, "Ameenda kuwa mgeni wa mtu mwenye dhambi."

8 Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana Isa, "Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango."

9 Ndipo Isa akamwambia, "Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu. 10 Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea."

Veja também