Isa amtakasa mtu mwenye ukoma
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Isa, akapiga magoti, akimwomba, "Ukitaka, unaweza kunitakasa."
41 Isa, akiwa amejawa na huruma, akaunyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, "Nataka. Takasika!" 42 Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.