Siku ya Mwenyezi Mungu
1 "Hakika siku inakuja, itawaka kama tanuru. Wote wenye kiburi na watenda maovu watakuwa mabua makavu, na siku ile inayokuja itawawasha moto," asema Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni. "Hakuna mzizi wala tawi litakalosalia kwao. 2 Bali ninyi mnaoliheshimu Jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mabawa yake. Nanyi mtatoka nje na kurukaruka kama ndama aliyeachiwa kutoka zizini.