22 Haya yote yalitukia ili litimie lile Mwenyezi Mungu alilonena kupitia nabii, aliposema: 23 "Tazama, bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, nao watamwita jina Imanueli" (maana yake, "Mungu pamoja nasi").
24 Yusufu alipoamka kutoka usingizini, akafanya jinsi alivyoagizwa na malaika wa Mwenyezi Mungu, akamchukua Mariamu kuwa mke wake. 25 Lakini hawakukutana kimwili hadi Mariamu alipojifungua mwanawe1:25 tafsiri zingine husema kifungua mimba; akamwita jina Isa.