Aliye mkuu katika Ufalme wa mbinguni
1 Wakati huo, wanafunzi wakamjia Isa na kumuuliza, "Je, nani aliye mkuu kuliko wote katika ufalme wa mbinguni?"
2 Isa akamwita mtoto mdogo na kumsimamisha katikati yao. 3 Naye akasema: "Amin, nawaambia, msipoongoka na kuwa kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika ufalme wa mbinguni. 4 Kwa hiyo mtu yeyote anyenyekeaye kama huyu mtoto, ndiye aliye mkuu kuliko wote katika ufalme wa mbinguni.