Isa amponya mwanamke na kumfufua msichana
18 Isa alipokuwa akiwaambia mambo haya, kiongozi wa sinagogi9:18 Nyumba ya ibada na mafunzo. akaingia, akapiga magoti mbele yake, akamwambia, "Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini njoo uweke mkono wako juu yake, naye ataishi." 19 Isa akaondoka akafuatana naye, nao wanafunzi wake pia wakaandamana naye.