20 Wakati huo huo, mwanamke mmoja, aliyekuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na mbili, akaja nyuma ya Isa, akagusa upindo wa vazi lake, 21 kwa maana alisema moyoni mwake, "Nikigusa tu vazi lake, nitaponywa."
22 Isa akageuka, naye alipomwona akamwambia, "Binti, jipe moyo, imani yako imekuponya." Naye yule mwanamke akapona kuanzia saa hiyo.