33 Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Mwenyezi Mungu, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Mwenyezi Mungu liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika. 34 Wingu la Mwenyezi Mungu lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
35 Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Musa alisema,
"Ee Mwenyezi Mungu, inuka!
Watesi wako na watawanyike;
adui zako na wakimbie mbele zako."
36 Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema,
"Ee Mwenyezi Mungu, rudi,
kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika."