12 Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na mtu wa Mataifa, yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao. 13 Kwa maana, "Kila mtu atakayeliitia Jina la Mwenyezi Mungu, ataokolewa."
14 Lakini watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Nao watawezaje kumwamini yeye ambaye hawajamsikia? Tena watamsikiaje bila mtu kuwahubiria? 15 Nao watahubirije wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, "Tazama jinsi ilivyo mizuri miguu yao wale wanaohubiri Habari Njema!"
16 Lakini si wote waliotii Injili. Kwa maana Isaya asema, "Mwenyezi Mungu, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?" 17 Basi, imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Al-Masihi.