19 Wapendwa, msilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu, maana imeandikwa: "Ni juu yangu kulipiza kisasi, nitalipiza," asema Mwenyezi Mungu. 20 Badala yake:
"Kama adui yako ana njaa, mlishe;
kama ana kiu, mpe kinywaji.
Kwa kufanya hivyo,
unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake."
21 Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.