Salamu kwa watu binafsi
1 Napenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe, mhudumu katika kundi la waumini la Kenkrea. 2 Naomba mpokeeni katika Bwana Isa ipasavyo watakatifu na kumpa msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, kwa maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, mimi nikiwa miongoni mwao.