Pular para o conteúdo
Publicidade

Sofonias 1

Siku kubwa ya Mwenyezi Mungu

14 "Siku kubwa ya Mwenyezi Mungu iko karibu:

iko karibu na inakuja haraka.

Sikilizeni! Kilio katika siku ya Mwenyezi Mungu

kitakuwa chungu.

Shujaa atapiga ukelele wa vita huko.

15 Siku ile ni siku ya ghadhabu,

siku ya fadhaa na dhiki,

siku ya uharibifu na ukiwa,

siku ya giza na utusitusi,

siku ya mawingu na giza nene,

16 siku ya tarumbeta na kelele za vita

dhidi ya miji yenye ngome,

na dhidi ya minara mirefu.

17 Nitawaletea watu dhiki,

nao watatembea kama vipofu,

kwa sababu wametenda dhambi

dhidi ya Mwenyezi Mungu.

Damu yao itamwagwa kama vumbi

na matumbo yao kama kinyesi.

18 Fedha yao wala dhahabu yao

hazitaweza kuwaokoa

katika siku hiyo ya ghadhabu ya Mwenyezi Mungu.

Katika moto wa wivu wake

dunia yote itateketezwa,

kwa maana ghafula ataleta mwisho

wa wote wanaoishi duniani."

Veja também

Sofonias
Ver todos os capítulos de Sofonias