16 Katika siku hiyo watauambia Yerusalemu,
"Usiogope, ee Sayuni;
usiiache mikono yako ilegee.
17 Mwenyezi Mungu, Mungu wako, yu pamoja nawe,
yeye ni Shujaa mwenye nguvu anayeokoa.
Atakufurahia kwa furaha kubwa,
atakutuliza kwa pendo lake,
atakufurahia kwa kuimba."